- 14,779 viewsDuration: 3:52Kesi ya mauaji ya mfanyabiashara Jayeshkumar Kanji Velji, aliyeuawa kikatili katika eneo la Lukenya mwaka 2024, imechukua mkondo mpya baada ya mshukiwa mmoja kuamua kushirikiana na upande wa mashtaka kwa kutaka kugeuzwa shahidi wa serikali. Shahidi huyo, ambaye ni mwendesha bodaboda, alieleza kwa mara ya kwanza matukio ya siku ya mauaji na kuwahusisha washukiwa wenzake na uhalifu huo. Ode Francis ana taarifa zaidi.