Kifo cha O.J. Simpson Marekani

  • | VOA Swahili
    252 views
    Nyota wa zamani wa Ligi ya Mpira wa Marekani NFL na mcheza filamu ambaye alifutiwa mashtaka ya mauaji ya mkewe na rafiki yake wa kiume katika kesi iliyoteka Marekani na dunia amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 76. O.J. Simpson amefariki baada ya kuugua ugonjwa wa saratani, kwa mujibu wa taarifa ya familia yake kwenye akaunti yake ya X. Gazeti la The Post lilisema kwamba alikufa siku ya Jumatano, akiwa amezungukwa na watoto wake na wajukuu. Ingawa Simpson hakukutwa na hatia ya vifo vya Nicole Brown Simpson na Ronald Goldman, miaka mitatu baada ya kesi hiyo ya jinai alipatikana na hatia ya kuwajibika katika kesi ya madai iliyofunguliwa na familia za waathirika. - Reuters #oj #simpson #nyota #nfl #football #mchezaji #star #voaswahili