Kuporomoka kwa daraja kuu la Baltimore, watu 20 watafutwa
Kikosi cha uokoaji na utafutaji kina endelea na zoezi la kuwatafuta watu 20 waliotoweka baada ya daraja kuu kubomoka katika mji wa Baltimore, Maryland ulioko kusini mwa Marekani
Video iliyochukuliwa kwa simu ya mkononi ilionyesha vipande kadhaa vya Daraja la Scott Key likiporomoka ndani ya maji ya Mto Patapsco baada ya meli iliyobeba mizigo yenye bendera ya Singapore inayoitwa Dali kugonga nguzo inayoshikilia daraja majira ya saa kumi na moja alfajiri (05:30 UTC) Jumanne.
Mamlaka zinasema magari kadhaa yalikuwa juu ya daraja wakati ajali hiyo ilipotokea.
Maafisa wa huduma za dharura wa Baltimore kikosi cha watafutaji na waokoaji kinaendelea kuwatafuta watu wasiopungua 20 ambao wanasadikiwa kuwa ndani ya maji.
Magari kadhaa yalianguka kwenye maji baridi na waokoaji walikuwa wakitafuta zaidi ya watu saba.
Wanasema vyombo vyao vimebaini kuna magari yaliyotumbukia mtoni.
Inaonekana Meli hiyo iligonga nguzo moja ya daraja Fransis scott key Bridge ambapo lilivunjika vipande, kulingana na picha zilibandikwa katika mtandao wa X.
Meli hiyo ilisababisha moto ulitoa moshi mweusi ulopaa hewani.
Meli hiyo inayosafiri na bendera ya Singapore na jina la Dali ilikuwa imeondoka bandarini dakika 25 zilizopita ikielekea Singapore.
Synergy Marine Corp, Wasimamizi wa meli ya Dali, wametoa taarifa wakisema meli hiyo iligonga moja ya nguzo za daraja hilo na kuwa mabaharia wake wote, wakiwemo nahodha wa meli hiyo wamesalimika na hakuna ripoti zozote za majeruhi.
Daraja hilo lenye urefu wa kilomita 2.5 lenye umri wa miaka 47 ni kiungo kikuu katika njia kuu zinazounganisha majimbo zinazo zunguka mji wa Baltimore, moja ya bandari kadhaa kubwa kabisa za Marekani.
Ilipewa jina la Francis Scott Key, mwandishi wa “The Star Spangled Banner,” shairi ambalo baadae lilitengenezwa kuwa muziki na hatimaye kuwa ni nyimbo ya taifa ya Marekani.
Key alihamasishwa kuandika shairi baada ya kushuhudia mashambulizi ya bomu yaliyofanywa na Uingereza katika ngome kuu ya jeshi la Marekani huko Baltimore mwaka 1814. - VOA NEWS, AP, Reuters
#Daraja #baltimore #kubomoka #magari #mtoni #francisscottkeybridge #marekani
11 Aug 2025
- Special trade agreements between Kenya and the UK allow the export of both goods and labour.
11 Aug 2025
- This comes a day after the case was reported at the Capitol Hill Police Station.
11 Aug 2025
- KUPPET claims that TSC should follow in the footsteps of the National Police Service.
12 Aug 2025
- Four reactors at France's Gravelines nuclear power plant were shut down late Sunday due to a swarm of jellyfish in the cooling systems, operator EDF said on Monday, likely due to rising water temperatures because of global warming.
12 Aug 2025
- The operator of Wikipedia on Monday lost a legal challenge to parts of Britain's Online Safety Act, which sets tough new requirements for online platforms and has been criticised for potentially curtailing free speech.
12 Aug 2025
- India's top court ordered authorities in the capital Delhi and its suburbs on Monday to relocate all stray dogs to shelters within eight weeks, according to the Live Law website, after media reports of a rise in cases of rabies, especially among…
12 Aug 2025
- President Donald Trump said on Monday that his administration is looking at reclassifying marijuana as a less dangerous drug and potentially lower criminal penalties, but no final decision has been made.
12 Aug 2025
- Nigerian prosecutors on Monday arraigned five men accused of carrying out a deadly Islamist militant attack on a Catholic church in Owo, in the southwestern Ondo state, that killed at least 50 worshippers in 2022 and wounded over 100 others.
12 Aug 2025
- The lakeside town is already abuzz with activity as visitors arrive from across the country, creating a windfall for local businesses and spilling demand into neighbouring counties.
12 Aug 2025
- The Police Service Commission, tasked with reforming the process, found itself under intense scrutiny from both civilians and serving officers, with many expressing concerns that the proposed system could disadvantage candidates from marginalized…
12 Aug 2025
- Farmers win round one as court halts duty-free rice importation
12 Aug 2025
- Equity to cool off State securities as half-year profit hits Sh34.6b
12 Aug 2025
- Fertiliser subsidy: A double-edged sword driving firms out of business