- 7,420 viewsDuration: 41sShughuli za usafiri zilitatizika hii leo jijini Nairobi, Kenya kufuatia mgomo wa wahudumu wa magari ya umma ya abiria maarufu kama matatu. Wahudumu hao ambao pia walifunga baadhi ya barabara wanalalamikia mtindo wa waendeshaji pikipiki maarufu kama bodaboda wanaochoma magari ya abiria baada ya ajali, badala ya kufuata sheria. Ni nini kimesababisha wahudumu hawa wa usafiri wa umma kugombana, na suluhu iko wapi? Kwa mengi zaidi, jiunge naye @midababirye katika Dira ya Dunia TV leo saa tatu usiku kupitia ukurasa wetu wa YouTube wa BBC Swahili. #bbcswahili #kenya #matatu Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili https://www.youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGw