- 95 viewsDuration: 2:43Maafisa tabibu katika kaunti ya Bungoma wamesitisha mgomo wao baada ya kuweka makubaliano mapya na serikali ya kaunti ya Bungoma. Wakizungumza baada ya kutia saini makubaliano hayo, naibu katibu wa kitaifa wa muungano huo Austin Odour, amesema kuwa maafisa hao wa kliniki wameitaka Serikali kutimiza makubaliano ambayo yameafikiwa. Serikali ya kaunti ya Bungoma imesema kuwa ni wajibu wao kuhakikisha kuwa wakazi wa Bungoma wanapata huduma za afya ipasavyo.