Maafisa wa polisi wanasa bangi katika eneo la Isebania mpakani Kenya na Tanzania

  • | Citizen TV
    576 views

    Maafisa wa polisi waliokuwa wakishika doria kando ya barabara kuu ya Migori - Isebania wamenasa bangi katika eneo la isebania mpakani Kenya na Tanzania.Bangi hiyo ilikuwa ikisafirishwa kwa gari kibinafsi. kamanda wa polisi Migori, Peter Kimani, alithibitisha kisa hicho na kueleza kwamba kunaswa kwa mihadarati hiyo, yenye thamani ya shilingi Milioni moja, iliwezeshwa kwa uhusiano kati ya wananchi na polisi.Kimani aliendelea kueleza kuwa watu waliokuwa ndani ya gari hilo waliamua kuliacha na kukimbia.