- 2,125 viewsDuration: 2:47Maafisa watatu wa kaunti ya Garissa wamefikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya kuilaghai kaunti hiyo shilingi milioni 51 zilizokusudiwa kununua chakula cha msaada kwa waathiriwa wa baa la njaa mwaka 2022. Miongoni mwa washtakiwa ni afisa wa maendeleo ya jamii katika kaunti hiyo ambaye alishtakiwa kwa madai kuwa kampuni yake ilitumika kupokea fedha hizo bila kuwepo kwa kandarasi halali wala kuwasilishwa kwa chakula chochote.