Madai ya sukari iliyoharibika kuuzwa Kenya yakanushwa

  • | KBC Video
    80 views

    Kampuni ya Mitchell Cotts imekanusha madai kwamba shehena ya sukari iliyonaswa na halmashauri ya bandari katika mabehewa yake mwaka jana inauzwa humu nchini. Mkurugenzi wa operesheni katika kampuni hiyo James Rarieya amesema sukari hiyo ilikuwa imeidhinishwa kuwa salama kwa matumzi iliposafirishwa kutoka Mauritius kabla ya meli iliyokuwa imebeba mabehewa hayo kupata hitilafu ilipotia nanga katika bandari ya Mombasa ambapo mabehewa 13 yalilowa maji na sukari hiyo kuharibika. Na kama anavyoripoti mwanahabari wetu Juney Karisa shirika la kitaifa la kukadiria ubora wa bidhaa limechukua sampuli kutoka zaidi ya magunia elfu 2 kabla ya sukari hiyo kuachiliwa kwa muagizaji.

    Connect with KBC Online; Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKN Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1 Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV Check our website: https://www.kbc.co.ke/

    #kbcchannel1 #news #kbclive