- 1,459 viewsDuration: 3:40Wakatoliki nchini wameshiriki jumatano ya majivu hii leo huku jumbe za kusikiliza, kufunga na kutenda mema zikishamiri. Maelfu ya wakatoliki na wakristo wengi duniani wakianza siku arobaini za kufunga na kuabudu. Kutwa nzima waumini wa kanisa la Holy Family Basilica hapa Nairobi walifanya misa ya majivu. Askofu wa kanisa katoliki jimbo la Nairobi philip anyolo aliyeongoza misa ya asubuhi akiwahimiza wanasiasa kukomesha siasa za mgawanyiko.