- 490 viewsMahakama kuu imesitisha kwa muda kuanzishwa kwa kituo cha Karantini kwa wagonjwa wa Ebola kwa raia wa marekani, kilichotarajiwa kujengwa katika kambi ya jeshi la wanahewa kaunti ya Laikipia. kesi hiyo iliwasilishwa mahakamani na taasisi ya katiba institute, ambapo serikali pia imekatazwa kuwapokea raia wa mataifa mengine waliougua ugonjwa huo hatari kwa matibabu. Aidha marekani imeahidi shilingi bilioni 1.7 kwa kenya za kukabiliana na ebola.