Wasichana walifanya vyema wakilinganishwa na wavulana kwenye matokeo ya tathmini ya shule ya sekondari msingi yaliyotangazwa leo huku waking’aa kwenye masomo 10 kati ya 12 yaliyotathminiwa.Waziri wa elimu Julius Ogamba, aliyetangaza matokeo hayo katika makao makuu ya baraza la kitaifa la mitihani, KNEC, alisema kuwa tathmini hiyo ambayo ni ya kwanza ya aina yake chini ya mtaala wa elimu ya umilisi itatoa mwongozo kuhusu mpito wa zaidi ya wanafunzi milioni- 1.13 hadi shule za upili. Waziri Ogamba, aliwahakikishia wazazi nchini kwamba wanafunzi hao wote watasajiliwa kwenye shule za upili na kwamba hakuna karo zozote zilizoongezwa.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive