- 1,303 viewsDuration: 2:58Huzuni na majonzi ilitanda katika eneo la Tseikuru, Kaunti ya Kitui wakati wa mazishi ya waathiriwa saba wa mashambulizi ya kikatili ya wiki iliyopita. Miongoni mwa saba hao ni ndugu wawili wa familia moja. Viongozi wametaka haki itendeke huku serikali ikiahidi kuweka mikakati ya kukomesha migogoro hiyo inayotokea mara kwa mara.