Mbunge Milemba wa Emuhaya afurushwa kwenye hafla baada ya kukiri kuunga mkono mswada wa fedha 2023

  • | Citizen TV
    375 views

    Mbunge wa Emuhaya Omboko Milemba alijipata taabani baada ya matamshi yake katika hafla ya michezo ya muungano ya walimu wa shule za upili KUPETT kaunti ya Homa-Bay. Zogo lilianza wakati mbunge huyo alijitambulisha na kusema alipga kura kuunga mkono mswada wa fedha katika bunge la kitaifa. Ni msimamo uliowaghadhabisha zaidi ya walimu 300 waliokuwa wakishiriki michezo hiyo na kumuamrisha aondoke. Licha ya Katibu Mkuu wa KUPPET Akello Misori kuwasihi walimu kuwa na subira, walimu hawa walisimama na azma yao wakisema mswada huo ni hatari kwao.