Meli ya mafuta ambayo ilikuwa ikiungua kwa wiki kadhaa katika Bahari ya Sham baada ya kushambuliwa na waasi wa Wahouthi wa Yemen, na kutishia kumwagika kwa mafuta imeokolewa, kampuni ya ulinzi imesema Ijumaa.
Meli hiyo Sounion ilikuwa ni maafa yanayo subiriwa kwa katika mkondo huo wa maji, huku ikiwa na mapipa milioni 1 ya mafuta ghafi ambayo ilishambuliwa na baadaye kuharibiwa kwa vilipuzi vilivyotumiwa na Wahouthi wanaoungwa mkono na Iran ikiwa ni sehemu ya kampeni yao juu ya vita vya Israel na Hamas huko Ukanda wa Gaza.
Ilichukua miezi kadhaa kwa waokoaji kuweza kuivuta meli hiyo, kuzima mioto na kushusha mafuta ghafi yaliyobaki..
“Mapema Oktoba, meli hiyo ilivutwa hadi upande wa kaskazini wa mfereji wa Suez ili kupakua mizigo, ambapo hivi sasa zoezi hilo limekamilika.”
Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani ilionya kuwa kuvuja kwa mafuta kutoka katika meli hiyo ya Sounion kungeweza kuwa “mara nne kwa ukubwa wa maafa ya Exxon Valdez” yaliyotokea mwaka 1989 nje ya pwani ya Alaska.
Hakuna maelezo yoyote ya mara moja kutoka kwa Wahouthi, ambao wamekuwa wakiushikilia mji mkuu wa Yemen, Sanaa, kwa zaidi ya muongo mmoja na wamekuwa wakipigana na ushirika wa unaongozwa na Saudi Arabia ambao unaiunga mkono serikali iliyo uhamishoni kwa muda mrefu. - AP
#wahouthi #meli #mafuta #bahariyasham #yemen
1 May 2025
- The 76-year-old born into a humble family of 10 children is the first clergyman from the west African country to receive a red hat, having been made cardinal in 2003 by John Paul II.
1 May 2025
- National Assembly Speaker Moses Wetang’ula has described Kasipul Member of Parliament Charles Were, who was shot dead on Wednesday evening in Nairobi, as a fearless and committed public servant.
1 May 2025
- In a Wednesday statement released by the Office of the Inspector General, the incident occurred at approximately 7:30 p.m. on Wednesday along Ngong Road, near the City Mortuary roundabout.
1 May 2025
- The defeated Democrat told supporters the apparent "chaos" of the last three months was actually the realization of a long-cherished plan by conservatives who are using Trump to twist the United States to their own advantage.
1 May 2025
- South Africa's President Cyril Ramaphosa is setting up a judicial commission of inquiry to establish whether attempts were made to prevent the investigation or prosecution of apartheid-era crimes, his office said on Wednesday.
1 May 2025
- Iran on Wednesday executed a man convicted of espionage for Israel's Mossad spy agency and involvement in the 2022 assassination of a Revolutionary Guards colonel, the judiciary said.
1 May 2025
- National Police Service (NPS) has launched investigations into the fatal shooting of Kasipul MP Charles Were, which occurred Wednesday evening
1 May 2025
- Swedish police detained a 16-year-old early on Wednesday on suspicion of murdering three people in a hair salon in the city of Uppsala, prosecutors said.