Mishahara na marupurupu yaathiri maendeleo nchini

  • | Citizen TV
    168 views

    Serikali sasa inasema kuwa hakuna nyongeza ya mishahara kwa wafanyakazi wa umma huku Mkuu wa utumishi wa umma Felix Koskei akisema kuwa nyongeza na marupurupu lazima yaambatane na hali ya uchumi. Akizungumza kwenye kongamano la kitaifa kuhusu mishahara, Koskei alielezea athari za gharama ya juu ya mishahara ya wafanyikazi wa serikali ambayo kwa sasa imezidi kiwango cha kisheria.