- 21 viewsRais wa Kenya William Ruto Alhamisi jioni alitangaza kifo cha Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Francis Ogolla, kilichotokana na ajali ya helikopta iliyotokea majira ya alasiri Kaskazini Magharibi mwa nchi. Akihutubia wanahabari katika ikulu ya Nairobi, Ruto alisema kuwa ndege hiyo ya kijeshi ilianguka eneo la Sindar kaunti ya Elgeyo Marakwet mwendo wa saa nane na dakika 20 alasiri. Ruto alisema watu wengine 9 pia walifariki katika ajali hiyo na kuongeza kwamba maafisa wengine wawili waliokuwa kwenye ndege hiyo walinusurika na wanaendelea kupatiwa matibabu hospitalini. Tisa hao ni pamoja na Brigedia Swale Saidi, Kanali Duncan Keittany, Luteni Kanali David Sawe, Meja George Benson Magondu, Kapteni Sora Mohamed, Kapteni Hillary Litali, Sajenti Mwandamizi John Kinyua Mureithi, Sajenti Cliphonce Omondi, na Sajenti Rose Nyawira. "Nina huzuni kubwa kutangaza kwamba Jenerali Francis Omondi Ogolla, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Kenya, amefariki” Rais Ruto alisema. Katika taarifa yake, Ruto alisema Ogolla aliondoka Nairobi Alhamisi asubuhi kuelekea kazini katika eneo la Bonde la Ufa, ambako alikagua ukarabati wa shule tano Elgeyo Marakwet. Pia alikuwa Turkana ambapo alikutana na kuzungumza na wanajeshi waliotumwa huko kabla ya kwenda Pokot Magharibi. Wakati wa ajali hii, Jenerali Ogolla na timu yake walikuwa wakielekea Kaunti ya Uasin Gishu. Kufuatia kifo cha Ogolla, Ruto ametangaza siku tatu za maombolezo huku bendera zikipepea nusu mlingoti. "Wakati huu wa maombolezo ya kitaifa, bendera ya Kenya, Bendera ya Jeshi la Ulinzi la Kenya, na bendera ya jumuiya ya Afrika Mashariki zitapepea nusu mlingoti katika balozi za Jamhuri ya Kenya na Kenya nje ya nchi," Ruto alisema. Uchunguzi umeanza kubaini kilichosababisha ajali hiyo. #mkuuwamajeshi #Jenerali #FrancisOgolla #rais #kenya #williamruto #ndege #jeshi #ajali #nairobi #voa #voaswahili
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Francis Ogolla Afariki katika Ajali ya Ndege
- 19 Jul 2025 - Germany said Friday it had deported 81 Afghan men convicted of crimes to their Taliban-controlled homeland, as Chancellor Friedrich Merz's government looks to signal a hard line on immigration.
- 19 Jul 2025 - A 15-month-old baby has died in Belgium after being left inside a car on a warm summer day, authorities said on Friday.
- 19 Jul 2025 - In 2022, the Central Bank of Kenya (CBK) put in place regulations to govern digital borrowing and lending, in efforts to provide better guidelines and experiences for consumers.
- 19 Jul 2025 - The Umoja na Maendeleo Party (UMP) under the leadership of former Meru Governor Kawira Mwangaza has announced its participation in the upcoming by-elections across Kenya. This move marks a significant step in Mwangaza’s political comeback following her…
- » Boniface Mwangi, Agather Atuhaire sue Tanzanian gov’t over alleged torture, seek Ksh.130M compensation19 Jul 2025 - Human rights activists Boniface Mwangi and Agather Atuhaire, alongside seven civil society organisations, have filed a case before the East African Court of Justice.
- 19 Jul 2025 - The building of sports stadiums worth Ksh6.17 billion has stalled, a new audit report shows. The report by the Auditor General, Nancy Gathungu, said there is no value for money as the projects have remained incomplete for a long time. The stadiums in…
- 19 Jul 2025 - Wiper Party leader Kalonzo Musyoka has issued a response dismissing reports suggesting a possible merger between his party and President William Ruto’s United Democratic Alliance (UDA). In a Facebook post on Friday, July 18, 2025, Kalonzo, in a brief…
- 19 Jul 2025 - Orange Democratic Movement (ODM) Communications Director Philip Etale has thrown his weight behind the ongoing community-based security initiative dubbed Jukwaa la Usalama, emphasising the need to tackle insecurity from the grassroots level. In a…
- 19 Jul 2025 - Interior Cabinet Secretary Kipchumba Murkomen has issued fresh directives to police officers on the use of force and firearms, particularly during public protests.
- 19 Jul 2025 - Since his meteoric rise to the Mining, Blue Economy and Maritime Affairs Cabinet Secretary position, Hassan Joho has increasingly asserted himself in Coast politics, rekindling a political presence that had momentarily dimmed. Political observers say…