Msemaji wa Iraq asema shambulizi la Marekani 'ni mauaji dhahiri'
Iraq siku ya Alhamisi imeikosoa vikali shambulizi lililofanywa na droni ya Marekani ambalo jeshi lake lilisema limemuua kiongozi wa kikundi cha wanamgambo kinachoungwa mkono na Iran.
Msemaji wa Iraqi ameliita shambulizi hilo “ni mauaji dhahiri” ambayo yanaonyesha “kutothamini maisha ya raia au sheria za kimataifa.”
Yehia Rasool, msemaji wa waziri mkuu wa Iraqi, alisema kuwa ushirika unaongozwa na Marekani ambao umekuwa na operesheni nchini Iraq kukabiliana na kikundi cha Islamic State “mara kwa mara imekwenda kinyume na sababu na malengo ya uwepo wake katika eneo letu.”
“Mwelekeo huo unailazimisha serikali ya Iraqi kuchukua hatua kuliko wakati wowote mwengine kusitisha kazi ya ushirika huu, ambayo imekuwa ni sababu ya kutokuwepo utulivu na kutishia kuingiza Iraq katika wimbi la vita,” Rasool alisema katika taarifa yake.
Kamandi Kuu ya Marekani, ambayo inasimamia operesheni za kijeshi za Marekani katika Mashariki ya Kati, ilisema kuwa shambulizi la Jumanne lililomuua kamanda wa kikundi cha wanamgambo Kataib Hezbollah ambaye “alihusika moja kwa moja kupanga na kushiriki katika mashambulizi dhidi ya majeshi ya Marekani katika kanda hiyo.”
Maafisa wawili wa Marekani wamethibitishia VOA kuwa kamanda huyo alikuwa ni afisa wa operesheni Wisam Mohammad al-Saedi. Picha katika mitandao ya kijamii zilidai kuonyesha kitambulisho chake cha Iraqi ambacho kilichomolewa kutoka katika mwili wake.
VOA mapema iliripoti kuwa jeshi la Marekani lilikuwa limehusika katika shambulizi la anga dhidi ya lengo lenye umuhimu wa juu katika Mashariki ya Kati lakini ilikuwa haijamtambua al-Saedi kwa jina lake.
Kanda ya video iliyokuwa imesambazwa katika mitandao ya kijamii inaonyesha gari moja lililokuwa linawaka moto katika barabara kuu ya Baghdad.
Shambulizi la Marekani lilikuwa kulipiza kisasi mashambulizi takriban ya droni 170, roketi na makombora yaliyotekelezwa dhidi ya majeshi ya Marekani huko Mashariki ya Kati tangu katikati ya Oktoba, mojawapo liliuwa wanajeshi watatu wa Marekani na kujeruhi wengine zaidi ya darzeni kaskazini ya Jordan wiki iliyopita.
Ripoti ya mwandishi wa VOA Chris Hannas
#Haifa #waelaldahdouh #hamzaaldahdouh #shirikalamwezimwekundu
#Rafah #Netanyahu #Misri #Hamas #Gaza #Palestina #IDF #GalMeirEizenkot #iran #iraq
12 Aug 2025
- The nominees will join several committees.
12 Aug 2025
- The Speaker has been on the detectives' radar.
12 Aug 2025
- The court is expected to provide further directions in the coming weeks.
12 Aug 2025
- Interior Cabinet Secretary Kipchumba Murkomen now says no public servant should openly oppose the government of the day, warning that such conduct is both illegal and unconstitutional.
12 Aug 2025
- DAP-K leader Eugene Wamalwa now says there is a plan by President William Ruto to infiltrate the political outfit through frivolous petitions seeking a change in leadership.
12 Aug 2025
- Long-delayed road projects in northern Kenya are set to resume after years of inactivity, Deputy President Kithure Kindiki has said, citing a new funding approach that has brought contractors back to site.
12 Aug 2025
- A woman has been arrested in Bondeni, Nakuru County for allegedly supplying cannabis and cannabis-laced cookies to minors in what authorities describe as a deliberate attempt to lure children into drug abuse.
12 Aug 2025
- The National Police Service Commission (NPSC) is facing mounting internal tensions that threaten to derail the planned recruitment of 10,000 new police officers this September.
12 Aug 2025
- The nominees will join several committees.
12 Aug 2025
- The DP said the decision by President William Ruto remains in force and is meant to do away with past discriminatory tendencies targeting some communities.
12 Aug 2025
- The Speaker has been on the detectives' radar.
12 Aug 2025
- Speaking during International Youth Day celebrations at Masinde Muliro University in Kakamega County, Dr. Ruto lauded the energy, creativity, and resilience of Kenyan youths, noting their influence in sectors such as science, technology, and sports.
12 Aug 2025
- The court is expected to provide further directions in the coming weeks.