Mshukiwa mkuu wa mauaji katika hospitali kuu ya Kenyatta Kennedy Kalombotole afikishwa mahakamani

  • | Citizen TV
    1,144 views

    Mahakama ya Kibera inatarajiwa kutoa mwelekeo kuhusu iwapo mshukiwa mkuu katika mauaji ya mgonjwa aliyeuawa hospitalini Kenyatta atazuiliwa kwa siku 21 ili kutoa nafasi ya uchunguzi. Wapelelezi wanadai kuwa huenda Kennedy Kalombotole akahatarisha maisha ya wengine iwapo atarejeshwa katika hospitali hiyo kwa matibabu. Haya yanajiri huku familia ya marehemu Edward Maingi ikitishia kuishtaki hospitali ya kenyatta kwa uzembe uliosababisha kifo cha mwana wao.