Mti wa kushangaza unaogeuka jiwe Tanzania

  • | BBC Swahili
    3,485 views
    Takribani nchi 10 duniani zinatajwa kuwa na aina hii ya miti ya kushangaza, inayoitwa Miti mawe. Tanzania ni moja ya nchi hizo. Kwa mujibu wa Wakala wa Huduma za Misitu nchini humo (TFS), miti hii inaweza kuishi miaka mpaka 150 kabla ya safari yake ya kugeuka jiwe inayochukua pia miaka na miaka. Mwandishi wa BBC Yusuph Mazimu, ametembelea kijiji cha Mbati, Kusini mwa nchi hiyo, katika mkoa wa Ruvuma, kijiji ambacho kwa mujibu wa TFS ni moja ya vijiji vichache duniani vyenye hifadhi kubwa ya miti hiyo. #bbcswahi #tanzania #misitu Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili https://www.youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGw