- 327 viewsDuration: 1:26Waziri wa Usalama Kipchumba Murkomen ametangaza mpango wa serikali wa kukipandisha hadhi Chuo cha Mafunzo cha Kiganjo kuwa chuo kikuu cha polisi. Ambapo maafisa wa polisi sasa wataweza kusomea kozi za shahada wakiwa katika maeneo yao ya utendakazi. Akizungumza alipokitembelea chuo hicho katika Kaunti ya Nyeri leo, Murkomen alisema serikali inaweka mikakati ya kuboresha vifaa na mafunzo ya polisi ili kukabiliana na changamoto za kiusalama za sasa.