Muungano wa walinzi wa kibinafsi unadai mishahara

  • | Citizen TV
    274 views

    Muungano wa Kitaifa cha Wafanyakazi wa walinzi wa Kibinafsi cha Kenya (KNPSWU) unashinikiza utekelezaji wa haraka wa nyongeza ya mishahara kwa walinzi wa kibinafsi kote nchini kama ilivyotangazwa na mamlaka ya udhibiti wa walinzi w akibinafsi. Maafisa wa muungano huo waliokutana Nairobi pia wanataka mazungumzo kati ya maafisa wote husika kutoka serikali kuu na muungano wa Cotu kutathmini usitishwaji wa michango ya wanachama kila mwezi kama ilivyoagizwa. Katibu mkuu wa cotu francis Awoli na mwenyekiti wa mamlaka ya udhibiti wa walinzi wa kibinafsi fazul mohammed wamerushiana cheche za maneno kuhusu makato ya wafanyikazi kwa cotu. Mamlaka hiyo iliamuru wafanyikazi wa mishahara ya chini zaidi walipwe shilingi elfu thelathini kila mwezi.