- 25,710 viewsDuration: 1:58Mvutano kati ya Marekani na China umeingia katika hatua mpya kufuatia kauli ya Donald Trump kusema ameruhusu meli za China kupita Mlango wa Hormuz baada ya ahadi ya China kwamba isisaidie Iran kijeshi. Hata hivyo, China imekanusha madai hayo na jeshi la Marekani limesema hakuna meli yoyote iliyoruhusiwa kupita hali inayozua mkanganyiko kuhusu ukweli wa taarifa hizo. Wakati huo huo, taarifa kutoka jeshi la Marekani zinaonyesha kuwa hakuna meli yoyote iliyoruhusiwa kupita katika njia hiyo muhimu ya usafirishaji, licha ya kauli ya rais. Mwandishi wa BBC Mariam Mjahid anaeleza #bbcswahili #China #marekani Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili https://www.youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGw