- 188 viewsDuration: 5:01Katika makala yetu ya mwanamke bomba wiki hii tunamuangazia Magdalene Stella Ramoya, mjane ambaye amechukua jukumu la kuwainua wajane wenzake katika kijiji cha Lwanya eneo la Matayos viungani mwa mji wa Busia. Kwa miaka kadhaa, Magdalene amekuwa kielelezo chema kwa wenzake anaowainua kupitia miradi mbalimbali na kuwapa matumaini ya kuendelea na maisha licha ya changamoto wanazokumbana nazo. Ni kutokana na juhudi zake ambazo zinawanufaisha zaidi ya wajane 5000 ambapo hii leo tunamvisha taji la mwanamke bomba.