- 1,171 viewsAliyekuwa mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IEBC), Wafula Wanyonyi Chebukati, aliaga dunia jana Alhamisi katika hospitali moja mjini Nairobi akiwa na umri wa miaka 63, baada ya kuugua kwa muda mrefu, kama ilivyothibitishwa na familia yake. Chebukati aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa IEBC mwaka 2017 na Rais wa wakati huo Uhuru Kenyatta. Kipindi chake kama mwenyekiti wa tume hiyo kilikumbwa na changamoto nyingi zikiwemo za kusimamia chaguzi za mwaka 2017 na 2022 zilizoghubikwa na utata. Matokeo ya uchaguzi wa urais wa 2017 yalibatilishwa na Mahakama ya Juu kwa sababu ya kasoro, na kusababisha uchaguzi wa marudio. Katika uchaguzi wa 2022, Chebukati alimtangaza William Ruto kama Rais mteule, akimshinda mpinzani wake wa karibu, Raila Odinga, huku kukiwa na mgawanyiko ndani ya tume hiyo. Makamishna wanne walipinga matokeo hayo na kusababisha mtafaruku mkubwa wa kisisa katika taifa hilio la Afrika Mashariki. Licha ya mzozo wa ndani na shinikizo kutoka nje, Chebukati aliendelea kutetea matokeo yaliyotangazwa, ambayo baadaye yaliidhinishwa na Mahakama ya Juu. Kipindi chake pia kilikumbwa na matukio ya kusikitisha, ikiwa ni pamoja na vifo vya maafisa wa IEBC Chris Msando 2017 na Daniel Musyoka 2022. Rais William Ruto aliomboleza kifo cha Chebukati akimtaja kuwa kiongozi aliyetumikia taifa kwa uadilifu, akisema kuwa kifo chake ni hasara kubwa kwa taifa. Chebukati ameacha mjane Mary Chebukati Wanyonyi, ambaye aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Ugavi wa Mapato 2023, na watoto kadhaa. - VOA Swahili #IEBC #WafulaWanyonyiChebukati #kifo #maombolezi #Rais #kenya #williamruto
Mwenyekiti wa zamani wa IEBC afariki akiwa na umri wa miaka 63
- 30 Apr 2025 - Kenya’s revised foreign policy is designed to address the interests of citizens and reposition Kenya's foreign engagements on the dynamic global landscape, Prime Cabinet Secretary Musalia Mudavadi has said.
- 30 Apr 2025 - President William Ruto’s State Visit to China saw more than 20 trade agreements and memoranda of understanding signed, that aim at improving various sectors of the economy.
- 30 Apr 2025 - The Climate Reality Project, a climate-focused nonprofit founded by former U.S. Vice President Al Gore, is set to host an in-person training event in Nairobi in June.
- 30 Apr 2025 - President William Ruto has praised the increased contributions to the National Social Security Fund (NSSF) as a step toward the country’s financial security.
- 30 Apr 2025 - The MCA is part of the numerous residents that have been the latest targets.
- 30 Apr 2025 - The new fees could prompt an increase in the prices of commodities.
- 30 Apr 2025 - President William Ruto has reaffirmed his commitment to transforming Kenya. He underscored his mission to implement lasting changes for the nation’s development. Speaking in Karen, Nairobi, during the installation of Dr Benard Chitunga as the Chancellor…
- 30 Apr 2025 - Motorists have been urged to cooperate with traffic marshals who will be present on site.
- 30 Apr 2025 - High Court Judge Bahati Mwamuye has declared a protest ban issued by former Nairobi Police Commander Adamson Bungei during the 2024 anti-tax demonstrations illegal and unconstitutional.
- 30 Apr 2025 - Justice Bahati Mwamuye issued the order in a case filed by the Law Society of Kenya (LSK), which had petitioned the court following the killing of Rex Masai during a protest.