- 118 viewsDuration: 3:44Mzee mmoja kutoka jamii ya Pokot ambae amekuwa mstari wa mbele kupigania amani katika eneo la ukanda wa kaskazini mwa Bonde la Ufa Wilson Lonapa ametuzwa kwa ukakamavu wake wa miaka mingi. Mzee Lonapa ambae hakuficha furaha yake anasema bado kuna safari ndefu ya kumaliza vita vya wizi wa ng'ombe na mauji ya kiholela ya watoto na kina mama eneo hilo.