- 5,358 viewsDuration: 2:20Wanaume wawili kutoka Aterait Teso Kusini wako mafichoni baada ya kushirikiana kumpiga shemeji yao mwanamke na kumuacha na majeraha mabaya ambayo yalisababisha kifo chake. Kulingana na majirani, inadaiwa kuwa, kumekua na mzozo kati ya mama na mkaza mwana huyo kwa muda, mzozo ambao uliwalazimu watuhumiwa kuingilia kati na kumuadhibu shemeji yao Ann Akalimat mwenye umri wa miaka 45 mama wa watoto watano ambaye aliaga dunia alipokua akipelekwa hospitalini. Familia ya marehemu imeiomba serikali kuwakamata washukiwa hao wa mauaji.