- 3,903 viewsDuration: 2:04Polisi wanachunguza taarifa za mawasiliano za mshukiwa mkuu ili kutanzua kitendawili cha kutoweka kwa mhasibu wa Chuo cha Uuguzi cha Kapenguria, Caroline Mokeira, aliyepotea katika njia ya kutatanisha mjini Kitale wiki mbili zilizopita. Maafisa kutoka Kitengo cha Upelelezi wa Jinai wanaendeleza uchunguzi huo wakiwa na matumaini ya kupata mwanga kuhusu kutoweka kwa mwanamke huyo ambaye hajaonekana tena tangu alipoondoka nyumbani na mumewe.