Rais asema Kenya iko kwenye mkondo wa ustawi kiviwanda

  • | KBC Video
    32 views

    Rais William Ruto amesema safari ya Kenya kuwa kitovu cha ustawi wa viwanda duniani iko kwenye mkondo bora. Rais Ruto amesema imani ya wawekezaji katika nchi hii imevutia uwekezaji mkubwa wa kigeni na pia kutoka humu nchini pamoja na kuinua hadhi ya nchi hii kiviwanda. Alisema hayo alipofungua rasmi eneo maalum la kiuchumi la mnada wa magari wa Jumbo Africa huko Naivasha ambalo ni la kwanza la aina yake kwa Wakenya na raia wa nchi za Afrika Mashariki kushiriki katika mnada huo mara mbili kwa mwezi wakitumia shilingi ya Kenya badala ya sarafu ya dola ya Marekani.

    Connect with KBC Online; Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKN Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1 Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV Check our website: https://www.kbc.co.ke/

    #kbcchannel1 #news #kbclive