- 4,512 viewsDuration: 3:53Marehemu mbunge wa emurua dikirr johana ng'eno atazikwa siku ya ijumaa nyumbani kwake Mogondu, kaunti ya Narok. Kamati ya kupanga mazishi imetangaza kuwa ibada ya wafu ya mbunge ng’eno na watu wengine watano walioangamia kwenye ajali ya ndege ya jumamosi itaandaliwa jumatano na alhamisi nairobi na pia katika kaunti ya Narok. Rais William Ruto ambaye alizuru makazi ya marehemu humo Karen hii leo kuomboleza na familia yake ametangaza kuwa serikali itasimamia gharama ya mazishi ya waathiriwa wengine wa mkasa huo.