- 62 viewsWaziri wa Elimu Julius Migos Ogamba Na Rais William Ruto wanasisitiza kuwa mpito wa wanafunzi wa gredi ya kumi umefikia asilimia 99. Hii ni licha ya takwimu kubaini kuwa hali sivyo na wanafunzi wakijitokeza kusimulia masaibu ya kushindwa kujiunga na sekondari ya juu. Wakizungumza kwenye kongamano la kitaifa la elimu huko Naivasha, rais ruto alirejelea msisitizo kuwa karo za shule zilipwe kupitia mfumo wa e-citizen ili kuzuia ufujaji wa fedha.