Rais William Ruto azuru shule ya msingi ya Joseph Kang'ethe siku ya pili ya KCPE na KPSEA

  • | Citizen TV
    481 views

    Rais William Ruto ameongoza maafisa wengine serikalini kushuhudia kuanza kwa mitihani ya KCPE na KPSEA siku ya pili. Rais Ruto alikuwa katika shule ya msingi ya Joseph Kangethe mtaani Kibera hapa jijini Nairobi na kuwahakikishia wakenya wote kuwa usalama umeimarishwa katika vituo vyote vya mitihani. Ruto amewataka maafisa wanaosimamia mitihani hiyo kuhakikisha kila mwanafunzi amepata mazingira mwafaka ya kufanya mtihani wao na pia kuhakikisha hakutakuwa na visa vya udanganyifu