- 7,240 viewsDuration: 16sTazama video inayomuonesha mwandishi wa habari akijikinga wakati milio ya risasi ikisikika karibu na Ikulu ya Marekani (White House), ambapo maafisa wa usalama walimpiga risasi mshukiwa ambaye baadaye alifariki dunia Raia mmoja aliyekuwa karibu na eneo hilo pia alijeruhiwa kwa kupigwa risasi wakati wa tukio hilo, huku Rais Donald Trump akiwa ndani ya White House lakini hakupata majeraha yoyote. “Tunaweza kuthibitisha kuwa wakati wa tukio hilo, raia mmoja pia alipigwa risasi. Hakuna afisa yeyote aliyejeruhiwa,” taarifa hiyo ilisema Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili https://www.youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGw