Russia iliionya Marekani kabla ya kufyatua kombora la Oreshnik
Msemaji wa Kremlin amesema leo Ijumaa kwamba Moscow iliipelekea Marekani onyo dakika 30 kabla ya kufyatua kombora jipya la masafa ya kati huko Ukraine.
Kremlin iliruhusu kufyatuliwa kombora hilo jipya lililopewa jina la Oreshnik dhidi ya mji ulio kati kati mwa Ukraine wa Dnipro jana alhamisi.
Rais Putin amesema kwenye hotuba yake kwamba shambulio hilo limefanyika kujibu hatua ya Kyiv wiki hii kutumia makombora ya Marekani na Uingereza yenye uwezo wa kufika mbali ndani ya Russia.
Putin alionya kwamba mfumo wa Marekani wa ulinzi wa anga hautaweza kuzuia kombora jipya ambalo anasema lina safiri kwa kasi ya mara 10 zaidi ya sauti.
Hii leo pia msemaji Peskov aliulaumu utawala wa hivi sasa wa Marekani kwa kuzorotesha ugomvi wa Ukraine na kusema kwamba hakuna mawasiliano kati ya Moscow na Washington juu ya suala hili. - AP
Wakati huo huo Waziri wa ulinzi wa Ukraine Rustem Umerov amesema serikali yake ilikuwa inaongeza uwezo wa ulinzi wa anga wakati ikijibu mashambulizi ya makombora ya masafa marefu ya Russia katika mji wa ukarine wa Dnipro.
Umerov ameyasema hayo leo katika maelezo yake kwa vyombo vya habari akiwa na mwenzake wa Sweden Pal Johnson mjini Stockholm.
Jonson ameongeza kuwa shambulizi la Russia haliwezi kuikatisha tamaa uungaji mkono wa serikali yake kwa Ukraine.
Alhamisi Russia ilifyatua makombora ya masafa marefu kujibu hatua ya Marekani na Uingereza kuiruhusu Kyiv kushambulia ndani ya ardhi ya Russia na silaha zake za Magharibi za ubora wa juu.
- AP and Reuters
#voaswahili #afrika #ukraine #russia #kombora #oreshnik #dnipro #moscow #russia
17 Jun 2025
- Gachagua has torn into President Ruto for what he terms as a disregard for human life.
17 Jun 2025
- The mask vendor was unarmed and shot in full glare of the public.
17 Jun 2025
- One person was shot by police at point-blank range, amid allegations police turned a blind eye to armed goons who attacked protesters.
18 Jun 2025
- KNCHR has recorded 22 casualties during the Tuesday demonstrations calling for the resignation of Deputy Police Inspector General Eliud Lagat over his alleged involvement in teacher Albert Ojwang's murder.
18 Jun 2025
- Today’s protests took a sinister turn as police officers and hired thugs joined forces in plain sight. In a scene both brazen and unsettling, hired goons arrived on motorbikes, others armed with clubs and whips terrorizing innocent passers-by all under…
17 Jun 2025
- What had been intended as protests to demand accountability over the murder of teacher Albert Ojwang in police custody last week turned into an all-out clash pitting three groups: the police, protesters and hired goons.
17 Jun 2025
- The police officer who shot an unarmed mask vendor during the demonstrations held in Nairobi on June 17, 2025, has been arrested.
17 Jun 2025
- At around 10 p.m. on a cold night, a sudden sharp pain on the right side of her stomach sent 22-year-old Vestina Samson to the ground. Writhing in pain, Vestina’s family was unsure how to help her.
17 Jun 2025
- Three officers, among them the Officer Commanding Station at Mawego Police Station, where the late Albert Ojwang’ was briefly held before his controversial transfer to Nairobi, have now recorded statements as investigations gather pace.
17 Jun 2025
- The streets of Nairobi on Tuesday were nothing short of lawless as police officers worked with goons to fight off protesters.
17 Jun 2025
- “The nation is reeling from the deeply troubling shooting of an unarmed civilian.”
17 Jun 2025
- The tragic road accident along the Bondo-Kisian road also left 30 others injured
17 Jun 2025
- Injuries range from gunshot wounds, head cuts, whip lashes and blunt trauma