- 724 viewsDuration: 2:50Rais William Ruto amesema mabadiliko katika mfumo wa ufadhili wa elimu ya juu yanaendelea, huku serikali ikinuia kutimiza ahadi ya kufadhili masomo ya wanafunzi wote wanaofuzu kujiunga na taasisi za elimu ya juu. Rais alisema hayo huku wanafunzi wakiendelea kutuma maombi ya ufadhili wa vyuo hivyo kupitia mfumo uliopo sasa, huku mashirika husika ya ufadhili yakisubiri bunge kupitisha mswada kuhusu mabadiliko hayo mapya. Brenda Wanga anatuarifu mengi.