Serikali yatoa wito kwa hospitali binafsi kupunguza gharama za matibabu ya figo
Serikali na hospitali binafsi nchini Tanzania zimetakiwa kutafuta njia za kupunguza gharama za matibabu ya figo na kuboresha huduma za Afya kwa wagonjwa wanaohitaji matibabu hayo.
Wakizungumza na Sauti ya Amerika baadi ya Wagonjwa na wadau wa afya wametoa wito huo kuhakikisha wagonjwa wa figo wanapata matibabu na kishauri matibabu hayo kuingizwa kwenye mfuko wa bima ya Afya.
Mariamu Mapinda ni mzaliwa wa Bariadi ambae ana tatizo la figo kwa kipindi cha muda mrefu ambalo limemfanya apate changamoto mbalimbali za kiafya ikiwemo kuvimba baadhi ya sehemu za mwili, mifupa kuishiwa nguvu pamoja na shinikizo la damu la mara kwa mara.
Mbali na kupata mtu wa kujitolea fogo, lakini gharama za upandikizaji pamoja na vipimo zimekuwa vikwazo vikubwa katika kufanikisha upandikizaji huo.
“ili niweze kurudi katika hali yangu na changamoto ninazopitia natakiwa kupandikiziwa figo lakini kuna gharama ambazo natakiwa kulipia. waliniambia kupandikiza figo gharama yake ni Millioni thelathini na vipimo kwa mtoaji figo itahitajika pesa nyengine” amesema Mapinda.
Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 9.1 mpaka asilimia 13.1 ya watu duniani wanaishi na magonjwa mbalimbali ya figo, kwa upande wa Tanzania asilimia 7 ya watu wanaoishi vijijini wanaishi na magonjwa ya figo na asilimia 15.5 ya watu wanaoishi mijini wanaishi na magonjwa mbalimbali ya figo.
Asia Mustapha kutoka Dar es Salaam ni mgonjwa wa figo na hapa anaeleza changamoto ambazo amekuwa akipitia ikiwemo dawa kuuzwa kwa bei kubwa na baadhi ya dawa hizo hazipatikani ndani ya nchi na kulazimika ziagizwe kutoka nje ya nchi.
Amesema “bei ya dawa zipo juu na vile vile kuna dawa nyingi ambazo hazipatikaniki. mfano hai ni mimi mwenyewe natakiwa kutumia dawa za kupandisha presha mimi presha yangu ni ya kushuka lakini dawa ya kupandisha presha haipatikani hivyo lazima niagize kutoka india kwahiyo wangapi wanaweza kuagiza kutoka nje.
Akizungumzia gharama za matibabu Dkt Saidi Kanenda ambaye ni Daktari bingwa wa magonjwa ya figo kutoka hospitali ya Bugando mkoani Mwanza amesema gharama kubwa ya matibabu ya figo hii yanatokana na vifaa vingi vinavyotumika kuagizwa kutoka nje ya nchi.
“Gharama ni kubwa na huwezi kumudu kwasababu huku kwetu hatutengenezi hivi vifaa kwahiyo tunategemea vifaa vya kununua kutoka nje ya nchi na hivyo vifaa vingine vinavyotumika vinatoka nje ya nchi na gharama yake ni kubwa” alieleza Dkt Kanenda.
Kauli mbiu ya mwaka huu inasema “Afya ya figo kwa wote, kuendeleza usawa katika ufikaji wa huduma na matumizi bora ya dawa”
Dkt Kanenda akiitaka serikali kuyaingiza matibabu ya figo katika mfumo wa bima ya Afya ili kuwasaidia wagonjwa wanaopitia changamoto hiyo kufanyiwa upandikizaji kirahisi na kuokoa gharama za kufanya uchujaji damu.
Imetayarishwa na Amri Ramadhani Sauti ya Amerika, Dar es Salaam.
#figo #matibabu #gharama #wagonjwa #ushauri #hospitali #bugando #muhimibili
11 Aug 2025
- Special trade agreements between Kenya and the UK allow the export of both goods and labour.
11 Aug 2025
- This comes a day after the case was reported at the Capitol Hill Police Station.
11 Aug 2025
- KUPPET claims that TSC should follow in the footsteps of the National Police Service.
12 Aug 2025
- Four reactors at France's Gravelines nuclear power plant were shut down late Sunday due to a swarm of jellyfish in the cooling systems, operator EDF said on Monday, likely due to rising water temperatures because of global warming.
12 Aug 2025
- The operator of Wikipedia on Monday lost a legal challenge to parts of Britain's Online Safety Act, which sets tough new requirements for online platforms and has been criticised for potentially curtailing free speech.
12 Aug 2025
- India's top court ordered authorities in the capital Delhi and its suburbs on Monday to relocate all stray dogs to shelters within eight weeks, according to the Live Law website, after media reports of a rise in cases of rabies, especially among…
12 Aug 2025
- President Donald Trump said on Monday that his administration is looking at reclassifying marijuana as a less dangerous drug and potentially lower criminal penalties, but no final decision has been made.
12 Aug 2025
- Nigerian prosecutors on Monday arraigned five men accused of carrying out a deadly Islamist militant attack on a Catholic church in Owo, in the southwestern Ondo state, that killed at least 50 worshippers in 2022 and wounded over 100 others.
12 Aug 2025
- The lakeside town is already abuzz with activity as visitors arrive from across the country, creating a windfall for local businesses and spilling demand into neighbouring counties.
12 Aug 2025
- The Police Service Commission, tasked with reforming the process, found itself under intense scrutiny from both civilians and serving officers, with many expressing concerns that the proposed system could disadvantage candidates from marginalized…
12 Aug 2025
- Farmers win round one as court halts duty-free rice importation
12 Aug 2025
- Equity to cool off State securities as half-year profit hits Sh34.6b
12 Aug 2025
- Fertiliser subsidy: A double-edged sword driving firms out of business