- 549 viewsDuration: 3:12Waziri wa afya Aden Duale ameelezea hofu kuhusu kuongezeka kwa maambukizi mapya ya virusi ya HIV hususan miongoni mwa vijana. Akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi zoezi la usambazaji wa dawa mpya ya kuzuia maambukizi ya HIV, Waziri Duale amesema kuwa licha ya hatua zilizochukuliwa kuhakikisha kuna dawa za kupunguza makali ya virusi hivyo, ipo haja ya kuwekeza zaidi katika mikakati ya kuhakikisha kuna kinga ya kutosha