- 9,822 viewsDuration: 2:41Shirika Moja la haki za kibinadamu la Marekani sasa limejiunga na viongozi, na wananchi wanaozidi kuuliza masuali na kuishtumu serikali kuhusiana na sakata ya utoaji wa pasipoti za kenya kwa watu wanaohusishwa na ukiukaji mkubwa wa haki za kibinadamu nchini Sudan. Shirika hilo lililo na makao yake makuu jijini New York, limeishtumu serikali kwa kuwapa pasipoti wafadhili wa vita nchini Sudan ambao wamewekewa vikwazo, pamoja na watu wanaohusishwa na wapiganaji wa kundi la Rapid Support Forces. Na kama anavyoarifu Brenda wanga, tetesi hizo zinazidi kutokota huku serikali ikisalia kimya kuhusu sakata hiyo.