Shule kote nchini zitafunguliwa kwa muhula wa pili kama ilivyoratibiwa

  • | KBC Video
    42 views

    Shule kote nchini zitafunguliwa kwa muhula wa pili kama ilivyoratibiwa licha ya mvua inayoendelea kunyesha, huku serikali ikisema imeweka mikakati ya kutosha kuhakikisha usalama wa wanafunzi. Jijini Nairobi, waathiriwa wa mafuriko ambao wametafuta hifadhi katika taasisi za masomo watahamishwa hadi kambi tatu maalum kwenye uwanja wa Masinde Muliro katika eneo la Huruma, kambi ya manaibu machifu ya Mavoko na Kasarani,sawia na maeneo mengine nchini. Lakini kutokana na mvua inayoendelea kunyesha, waathiriwa walioachwa bila makazi kutokana na mafuriko wanaelezea masaibu yao wakitoa wito kwa serikali kuingilia kati na kuepusha mzozo wa kibinadamu.

    Connect with KBC Online; Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKN Follow us on Twitter: https://twitter.com/KBCChannel1 Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1tv Check our website: https://www.kbc.co.ke/

    #KBCchannel1 #Kenya #News