- 194 viewsDuration: 3:57Imebainika kuwa licha ya mtaala wa CBE kuingia gredi ya kumi mwaka huu , bado ukosefu wa Miundomsingi hasa katika shule za mashinani ni changamoto kuu katika kutekeleza mtaala huo ambapo shule nyingi hazina vifaa hitajika. Wakizungumza wakati wa kuzindua madarasa ya masomo ya sayansi katika shule za msingi za Moipei na ile ya Piliwa zilizoko Kajiado ya kati wadau wa elimu wanasema Bado walimu na wanafunzi wanahangaika kutekeleza mtaala huo kutokana na kukosekana kwa vifaa na miundo msingi bora.