- 380 viewsRais wa zamani wa Marekani Donald Trump amesema Seneta wa Ohio James David Vance (JD) Vance, mwenye umri wa miaka 39, ndiye chaguo lake la mgombea mwenza kuelekea uchaguzi wa mwezi Novemba. Trump alisema kupitia ujumbe kwenye mtandao wa kijamii wa Truth Social: “Baada ya kutafakari na kufikiria kwa muda mrefu, na kwa kuzingatia vipaji vya hali ya juu vya wengine wengi, nimeamua kwamba mtu anayefaa zaidi kushika wadhifa huop ni JD Vance wa jimbo la Ohio." Kongamano la Kitaifa la Chama cha Republican lilianza wiki hii, huku wajumbe na maafisa wakiwasili mjini Milwaukee, Wisconsin wakati kukiwa na msukosuko uliofuatia jaribio la kumuua Trump Jumamosi. Trump anatarajiwa kuteuliwa rasmi kuwa mgombea urais kwa tikiti ya chama cha Republikan. Shirika la habari la AFP linaripoti kuwa kupanda kwa J.D. Vance hadi mgombea mwenza wa Donald Trump kunakamilisha mabadiliko makubwa kwa seneta huyo, ambaye sasa anaonekana kuwa sura ya baadaye ya chama cha Republican. Vance amekuwa mmoja wa watatezi wakubwa wa Trump katika bunge, akiunga mkono sera mbalimbali zenye utata kama vile kupinga uhamiaji, kusisitiza Ukristo kama njia ya kukuza maadili ya umma na ya kibinafsi, na kupinga vita vya Ukraine dhidi ya uvamizi wa Russia. Mapema mwaka huu, seneta huyo wa Ohio alionya wale ambao hawamuungi mkono Trump kwamba "ana kumbukumbu ya muda mrefu." "Kama unampinga Trump na wale anaowaunga mkono, usitegemee msaada wangu," alisema. Hata hivyo, Vance katika siku za nyuma alikuwa mkosoaji wa Trump, na wakati mmoja alimuita "Hitler wa Marekani," kwa mujibu wa shirika la habari la AFP. #donaldtrump #marekani #republikan #chama #jdvance #jimbo #ohio #milwaukee #wisconsin #raiswazamani
Trump amteua Seneta JD Vance kuwa mgombea mwenza
- - Kenya-Finland Ties ››
- 14 May 2025 - Sean "Diddy" Combs' former girlfriend, Casandra Ventura, the star prosecution witness at the hip-hop mogul's sex trafficking trial, testified on Tuesday that her music career began to suffer as she increasingly spent her time participating in days of…
- 14 May 2025 - South Africa's unemployment rate rose in the first quarter of this year, with statisticians fretting that increasing numbers of people appear to have given up looking for work.
- 14 May 2025 - Israeli Prime Minister Benjamin Netanyahu said the military will enter Gaza "with full force" in the coming days, despite ongoing ceasefire efforts and the release of a US-Israeli hostage from the war-ravaged territory.
- 14 May 2025 - Finland President Alexander Stubb has hailed the historical Kenyan Gen Z movement witnessed in June last year during the anti-government protests, saying it was a momentous display of democracy.
- 14 May 2025 - Opposition leaders are now claiming that the Independent Electoral and Boundaries Commission (IEBC) nominees presented to Parliament for approval to take up management of the electoral body are a project to rig the 2027 General Election.
- 14 May 2025 - The crisis in the country's education sector continues to deepen, with the latest development being a Ksh.62 billion budget shortfall.
- 14 May 2025 - Tanzanian authorities arrested a senior opposition official as he was departing for a political conference in Belgium, his party said on Tuesday, as fears grow of an escalating crackdown ahead of an October election.
- 14 May 2025 - “No clean water. No toilets. No electricity. No well-planned living environment.” That is how Pastor Evans Moseti describes the one-room mabati house he has called home for the past nine years, its blue iron-sheet walls barely holding back Nairobi’s…
- 14 May 2025 - Court: Muturi resigned, not fired as Ruto claimed
- 14 May 2025 - Public participation on Finance Bill begins