Uganda: Kiongozi wa upinzani awekwa katika kizuizi cha nyumbani mara baada ya kuwasili nchini

  • | VOA Swahili
    219 views
    Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Bobi Wine amesema siku ya Alhamisi amewekwa katika kizuizi cha nyumbani, baada ya kukamatwa na maafisa wa usalama alipokuwa akirejea nyumbani akitokea nje ya nchi. Wine, mwanamuziki maarufu aliyegeuka kuwa mwanasiasa aliyeshindana na Rais mkongwe Yoweri Museveni katika uchaguzi uliopita wa mwaka 2021 nchini Uganda, amekuwa akikamatwa mara nyingi. "Walinikamata kinyume cha sheria kama ulivyoona, na tunapozungumza hivi sasa niko chini ya kizuizi cha nyumbani. Wanajeshi na polisi wako kila mahali," Wine aliwaambia waandishi wa habari nyumbani kwake kaskazini mwa mji mkuu Kampala. "Mara tu nilpotua wahuni walinikamata, waliniburuza, walinikunja mikono yangu na kunifungia kwenye gari binafsi lililokuwa likisubiri. Walinieleka hadi kwenye uwanja wa ndege wa zamani ambako walinitoa na kuniweka kwenye gari la kijeshi lililokuwa na wanajeshi wengi na maafisa wa polisi. "Ilikuwa inadhalilisha sana," alisema Wine, ambaye jina lake halisi ni Robert Kyagulanyi. Bobi Wine pia amesema kuwa wafuasi wake 300 wamekamatwa, lakini hakutoa maelezo zaidi na AFP haikuweza kpata uthibitisho huru. Polisi walikanusha kuwa Wine alikamatwa, walisema walikuwa "walimsindikiza" kijana huyo mwenye umri wa miaka 41 kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe kwenda nyumbani kwake. Chanzo cha habari hii ni Shirika la habari la AFP - - - - - #VOASwahili Sauti ya Amerika - Idhaa ya Kiswahili inawafikia zaidi ya watu milioni 100 wanaotembelea tovuti, mitandao ya kijamii, radio na televisheni zetu. Tunawasilisha maudhui kuhusu Afrika Mashariki na Kati kwa nchi takriban 11 huko Afrika na wale walioko ughaibuni na kwingineko duniani. Vipindi vyetu vimejikita katika maudhui mbalimbali ikiwemo habari, vijana, wanawake, siasa, sayansi, teknolojia, afya, biashara, michezo, muziki na burudani na pia tunawashirikisha wasikilizaji wetu.