- 111 viewsDuration: 1:24Ujenzi wa kituo cha Viwanda huko Kirinyaga unakaribia kukamilika, hii ikiashiria hatua muhimu katika safari ya kaunti hiyo kuelekea kuwa kitovu cha kikanda cha usindikaji wa bidhaa za kilimo na maendeleo ya viwanda. Kituo hicho, ambacho kiko ndani ya mji wa viwanda na kilimo wa Sagana, kitasaidia kuongeza thamani, kuimarisha mifumo ya thamani ya kilimo na kuunda fursa za ajira. Kulingana na usimamizi wa kaunti ya Kirinyaga, Kwa sasa, ujenzi wa maghala manane umekamilika kwa asilimia 86.