Upinzani wasema utamwondoa Rais Ruto mamlakani

  • | Citizen TV
    8,978 views

    Vinara wa upinzani wamemkashifu rais William Ruto kwa msamaha alioutoa jana kwa vijana nchini kwa madhila waliyopitia kufuatia maandamano ya kizazi cha Gen Z, wakidai kwamba msamaha huo ulikuwa wa unafiki. Vinara hao ambao wamezungumza nyumbani kwake kinara wa wiper Kalonzo Musyoka huko Tseikuru kaunti ya Kitui, wamemtaka Rais kuashiria kwa vitendo kughadhabishwa kwake na matukio ya mwaka uliopita kwa kuhakikisha walioumia na wale waliofariki wamepata haki la sivyo msamaha alioomba hauna msingi. Katika kikao cha Leo kilicholeta pamoja vinara wa vyama tofauti, aliyekuwa Naibu rais Rigathi Gachagua amemtaka aliyekuwa bosi wake kujiandaa kufunganya virago vya kuondoka ikuluni mapema, akidai kuwa kikosi hicho tayari kimeandaa mipango kabambe ya kumtimua.