Vifaru vya Israeli vikifanya mashambulizi karibu na mpaka wa Israel na Gaza

  • | VOA Swahili
    1,895 views
    Mashambulizi ya Israeli yamepiga katikati ya Gaza Jumanne (Desemba 26) baada ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kuahidi kutositisha mashambulizi dhidi ya Hamas, huku wakazi wa pwani wakiomboleza vifo zaidi katika vita ambavyo vimeuwa zaidi ya Wapalestina 20,000. Israel imedhamiria kuendelea mpaka ifikie lengo lake la kuiangamiza Hamas licha ya wito wa kimataifa kuwepo kwa kusitishwa mapigano katika wiki ya 11 ya vita hivyo, huku wasiwasi kuhusu mgogoro huu kuweza kuenea ukiyahusisha majeshi ya Marekani na Iran kushambuliana sehemu nyingine katika eneo hilo. Tangu Hamas ilipofanya shambulizi la kinyama dhidi ya Israel katika historia ya miaka 75 ya nchi hiyo, Netanyahu amejibu shambulizi hilo kwa nguvu zote za kivita dhidi ya eneo la Gaza linalotawaliwa na Hamas. Siku ya Jumanne, majeshi ya Israeli yalisema wanajeshi wake 160 hadi sasa wameuawa huko Gaza tangu operesheni ya kijeshi ya ardhini ilipoanza Oktoba 20. - Reuters #Rafah #Netanyahu #Misri #Hamas #Gaza #Palestina #IDF #GalMeirEizenkot #GadiEizenkot #wazirimkuu