- 219 viewsDuration: 3:16Kadri teknolojia ya kidijitali na akiliunde zinavyoendelea kubadili elimu na soko la ajira, Kaunti ya Wajir imehitimisha mafunzo ya siku nne ya ujuzi wa kidijitali yaliyowanufaisha wanafunzi 600 na vijana 200 walio nje ya mfumo wa elimu. Mafunzo hayo yalilenga kuwapa ujuzi wa kidijitali, matumizi salama ya mtandao na kuwaandaa kwa fursa za ajira na ujasiriamali.