- 983 viewsDuration: 3:00Viongozi wa Kaunti ya Trans Nzoia wanaitaka halmashauri ya kutathmini utendakazi wa polisi Independent Policing Oversight Authority (IPOA) kufanya uchunguzi wa kina kuhusu operesheni inayoendelea kunasa magenge ya wahuni katika eneo hilo. Viongozi hao wanadai kuwa operesheni hiyo haiendeshwi kwa mujibu wa sheria na kwamba inakiuka haki za kimsingi za wananchi. Na kama anavyoarifu Collins Shitiabayi, maafisa wawili wakuu katika ofisi ya Gavana wa Kaunti ya Trans Nzoia George Natembeya walikamatwa jana kwa tuhuma za kuhusika na uhuni.