- 346 viewsDuration: 1:57Viongozi wa kidini kutoka Kaunti ya Kajiado wamekemea ongezeko la uvamizi na vurugu kanisani, wakisema linatishia uhuru wa kuabudu, amani na Utangamano wa kitaifa. Viongozi hao Wamesisitiza kuwa maeneo ya ibada yanapaswa kulindwa wakati wote na kuzitaka idara za usalama kuwafikisha mahakamani wanaohusika na mashambulizi dhidi ya makanisa.Aidha wameeleza wasiwasi wao kuhusu visa vya kutekwa nyara kwa vijana, wakiitaka serikali ichunguze matukio hayo na kuwachukulia hatua za kisheria wahusika.