- 2,401 viewsDuration: 2:06Viongozi wa kisiasa kutoka eneo la Pwani Sasa wanamtaka Rais William Ruto kumteua waziri wa Madini Ali Hassan Joho kama mgombea mwenza wake kwenye uchaguzi wa 2027. Wakizungumza mjini Malindi kaunti ya Kilifi, wanasiasa hao wakiongozwa na naibu kinara wa chama Cha ODM, gavana wa kaunti ya Mombasa Abdswamad Nassir wanasema Joho ana tajirba ya kutosha Kwa wadhifa huo.Viongozi hao wanasema kwa muda mrefu eneo hilo limekuwa likipata mawaziri na makatibu wa wizara mbali mbali na kwamba muda umefika Sasa eneo hilo kutoa naibu rais wa taifa hili. Aidha wanasisitiza kuwa kwenye mazungumzo baina ya chama Cha Chungwa na kile Cha UDA, suala la mgombea mwenza sharti lipewe kipaumbele.