- 7,016 viewsDuration: 3:13Wanasiasa wa mrengo wa ODM wa Linda Mwananchi wamewasilisha malalamishi kwa Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI) wakidai kulengwa kwa wafuasi wao. Malalamishi hayo yaliwasilishwa na Gavana wa Siaya James Orengo na Mbunge wa Embakasi East Babu Owino wakidai kuwepo kwa kitengo maalum cha polisi kuwalenga wafuasi wao Kisumu. Aidha, viongozi hao wamewalaumu maafisa wakuu wa usalama kwa mchipuko wa magenge.