- 212 viewsDuration: 1:51Visa vya utapiamlo miongoni mwa watoto katika kaunti ya Garissa vimeongezeka zaidi wakati huu hali ya ukame inaposhuhudiwa na kufikia 13.6%. Kwenye mkutano ya wakuu wa sekta mbalimbali wa kaunti hiyo ulioandaliwa na shirika la WISER wa kuimarisha viwango vya kukabiliana na majanga hayo, takwimu zinaonyesha kuwa kati ya watoto kumi, wawili wanakabiliwa na tatizo la utapiamlo kaunti hiyo.